JUA KWANINI NIYONZIMA ASEMAYANGA HAIMTISHI WALA HAIMPI HOFU NA KUIPONGEZA SIMBA
Na Joseph michael Haruna niyonzima mchezaji wa SIMBA lakini kabla ya hapo alikuwa akiichezea timu pinzani ya SIMBA yani YANGA ambako mwanzoni mwa msimu huu wa 2017/2018 Niyonzima alihamia SIMBA.Pamoja na kuanza msimu kwa kiwango kisicho ridhisha akiwa SIMBA Haruna Niyonzima pia alikuwa nnje ya uwanja kwa muda mrefu baada ya kuumia. Lakini habari njeema kwa mashabiki na wapenzi wa SIMBA ni kwamba Niyonzima amerudi uwanjani na ameanza kufanya mazoezi na timu na pia si ajabu tukashuhudia akiecheza mechi ya SIMBA NA NJOMBE MJI ambayo itachezewa mjini njombe. Baaada ya kufanya mahojiano na CLOUDS FM jana Niyozima alizungumzia mambo mengi sana pamoja na kuelezea hali yake ya kiafya kuimarika vizuri na kuwa teyari kuingia uwanjani japo kuwa alikumbusha kwamba kuhusu maelekezo au nafasi ya kucheza bahado yanategemea sana namna ambavyo mwalimu atapanga mipango yake na daktari wa timu atakavyo elekeza au shauri.Na pia hakusita kuipongeza timu yake ya SIMBA kwa kufanya vizuri kwenye ligi h...