Posts

Showing posts with the label Kutoka magazetini

YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO MARCH 30 BARANI ULAYA

Image
Na Yego Sholla  Manchester City wanaamini wanaweza kusaini makataba na mchezaji wa kiungo cha kati wa Real Madrid Mhispania Isco msimu huu wa majira ya joto. Mkataba kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 unaweza kuwa wa thamani ya Euro milioni 75. (Mirror) Mchezaji wa kiungo cha kati wa Ubelgiji Mousa Dembele, mwenye umri wa miaka 30, hatasaini makataba mpya na Tottenham kabla ya Kombe la Dunia la mwaka huu, na hivyo kuibua maswali kuhusu mustakabali wake katika klabu hiyo. (Telegraph) Mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski, mwenye umri wa miaka 29, atawasilisha maombi yake ya kutaka kuhamia Real Madrid msimu huu wa majira ya joto. Mchezaji wa Chelsea mwenye umri wa miaka 25 na mchezaji wa kimataifa wa Uhispania Alvaro Morata ni mmoja wa washambuliaji ambao Bayern Munich inamtaka kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Pole iwapo watampoteza. (AS - in Spanish) Mchezaji wa kiungo cha kati wa Paris St-Germain midfielder Hatem Ben Arfa ametangaza kuwa ataondoka ka...

YASEMAVYO MAGAZETI BARANI ULAYA LEO MARCH 19

Image
Na Yego Sholla Real Madrid imekubali mkataba wa kumsajili mshambuliaji wa Poland Robert Lewandowski, 29, kutoka Bayern Munich msimu ujao . (Mundo Deportivo - in Spanish) Burnley iko tayari kuongeza mshahara wa kipa Nick Pope ili kuizuia Newcastle United kumnyatia. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ambaye ameitwa katika kikosi cha Uingereza kwa mara ya kwanza kwa sasa analipwa mshahara wa £15,000 kwa wiki hukoTurf Moor. (Sun) Manchester United imeongeza kandarasi ya miezi 12 ya beki Ashley Young, 32, katika klabu hiyo hadi 2019. (Mail) Takriban wachezaji 10 wa Manchester United katika kikosi cha kwanza akiwemo Michael Carrick, 36, anayestaafu na kiungo wa kati ambaye kandarasi yake imekwisha Marouane Fellaini, 30, pamoja na Zlatan Ibrahimovic, 36, huenda wakaondoka Old Trafford msimu huu (Express) Takriban wachezaji 10 wa Manchester United katika kikosi cha kwanza akiwemo Michael Carrick, 36, anayestaafu na kiungo wa kati ambaye kandarasi yake imekwisha Marouane Fella...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO KUTOKA MAGAZETINI JUMANNE YA MARCH 13

Image
Na Yego Sholla Aliyekuwa mkufunzi wa Watford Marco Silva ni miongoni mwa wakufunzi wanaopigiwa upatu kuchukua kazi ya kuikochi Southampton kufuatia hatua ya klabu hiyo kumfuta kazi kazi kocha wake Mauricio Pellegrino siku ya Jumatatu.. (Mail) Chelsea inamnyatia kipa wa AC Milan Gianluigi Donnarumma, 19, iwapo kipa wa Ubelgiji Thibaut Courtois, 25, ataondoka Stamford Bridge. (Corriere dello Sport, via Talksport) Newcastle itajaribu kumsajili winga wa Chelsea aliyepo katika klabu hiyo kwa mkopo kwa mkataba wa kudumu lakini italazimika kulipa hadi £15m kumnunua mchezaji huyo wa Brazil ,mwenye umri wa miaka 22. (Mirror) Newcastle, Leicester na Southampton wanamtaka winga wa Burnley mwenye umri wa miaka 27 Johann Berg Gudmundsson. (Sun) Barcelona imekuwa ikimnyatia kwa miezi kadhaa sasa mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 26, baada ya mchezaji huyo kutokubaliana na Atletico Madrid kuhusu kuongezewa kandarasi yake. (Le10sport.com - in French) Mkufunzi wa West Brom Alan ...