YASEMAVYO MAGAZETI YA LEO MARCH 30 BARANI ULAYA
Na Yego Sholla Manchester City wanaamini wanaweza kusaini makataba na mchezaji wa kiungo cha kati wa Real Madrid Mhispania Isco msimu huu wa majira ya joto. Mkataba kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 unaweza kuwa wa thamani ya Euro milioni 75. (Mirror) Mchezaji wa kiungo cha kati wa Ubelgiji Mousa Dembele, mwenye umri wa miaka 30, hatasaini makataba mpya na Tottenham kabla ya Kombe la Dunia la mwaka huu, na hivyo kuibua maswali kuhusu mustakabali wake katika klabu hiyo. (Telegraph) Mshambuliaji wa Bayern Munich Robert Lewandowski, mwenye umri wa miaka 29, atawasilisha maombi yake ya kutaka kuhamia Real Madrid msimu huu wa majira ya joto. Mchezaji wa Chelsea mwenye umri wa miaka 25 na mchezaji wa kimataifa wa Uhispania Alvaro Morata ni mmoja wa washambuliaji ambao Bayern Munich inamtaka kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Pole iwapo watampoteza. (AS - in Spanish) Mchezaji wa kiungo cha kati wa Paris St-Germain midfielder Hatem Ben Arfa ametangaza kuwa ataondoka ka...