WAAMUZI WA KIINGEREZA KUTOWEPO URUSI.
Na Yego Sholla Kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 80, nchi ya Uingereza haitakuwa na mwamuzi kwenye michuano ya kombe la dunia. Lakini ni UK nzima kwa maana ya Uwelshi, Uskochi, na Jamhuri ya Ireland. Lakini gumzo kubwa lipo Uingereza maana hata kiuwezo lenyewe ni taifa kubwa kimpira ukilinganisha na hayo mengine. Wana ligi inayofuatiliwa zaidi na wamekuwa na kawaida ya kuamini kuwa ubora wote uko kwao pia. Promo na vitu kama hivyo na ndio maana kuna mshtuko miongoni mwa wengi kuwa hawana hata mwamuzi mmoja kwenye michuano hii. Sababu ambayo wengi watakupa ni kwamba ubora wa waamuzi kutoka nchini humo umepungua. Hili linaweza kuwa kweli lakini hebu tuangalie vizuri na mengine. Kikawaida mwamuzi huwa anasemekana kufikia kilele cha uamuzi pale anapofanikiwa kuchezesha fainali ya michuano mikubwa zaidi ya soka Ulimwenguni. Na hili huwa liko wazi kutokana na ubora wa mwamuzi husika kwenye kuchezesha soka la ngazi mbali mbali hapo kabla. Hivyo basi waamuzi kutoka Uingereza ndio wam...