Griezmann nakwenda Barcelona

Taarifa za hivi punde kutoka Sky Sports na Ulimwengu wa soka Tz zinasema  mwendo huu nadhani Uongozi wa klabu ya Barcelona utazidi kuongeza kasi ya kumsajili straika wa kimataifa wa Ufaransa Antoine Griezmann kutoka Atletico Madrid.

Mwanaume amefunga magoli saba katika mechi mbili zilizopita , baada ya hapo jana kuwatungua Leganes magoli manne peke yake na Jumapili aliwatungua Sevilla magoli matatu peke yake.

Na hatimaye ameiwezesha timu yake kupunguza pointi dhidi ya vinara Barcelona na kuwa 4 , huku Barcelona wakicheza mechi yao moja ya mkononi usiku wa leo dhidi ya Las Palmas ,na siku ya Jumapili vilabu hivyo viwili ( Barcelona Vs Atletico Madrid ) vitashindana ubavu katika dimba la Nou Camp.

Comments

Popular posts from this blog

Njia sahihi za kuachana na unywaji wa pombe