Dondoo za Usajili Tanzania na nje ya Tanzania

Hatma ya Haruna Niyonzima Kujulikana wiki Ijayo , Simba yasema Haiwezi Ongelea Juu ya hilo tena kwani mwenye macho ataona na mwenye masikio atasikia .

Ndanda FC imesema kwamba Wataangalia Uwezekano Wa Kumnasa , Julio awe kocha wao mkuu .

Yanga yasema bado Hawajamaliza Usajili , Wasikika wakisema Watashusha Vifaa pale Itakapo bidi .

Mkude asema Kwamba Hawezi kuongelea sana Usajili Unaofanywa Klabuni hapo ila muda Utaongea .

Za kimataifa

Sunderland imemtangaza Simon Gryson kuwa kocha mkuu Wa Klabu hiyo na kumpa kandarasi ya miaka 3 .

Klabu ya Deportivo Alaves ya nchini Hispania imefanikiwa kunasa Saini ya mtoto Wa kocha Zinedine Zidane  Wa kuitwa Enzo Zidane na kumpa kandarasi ya miaka 3 akitokea Real Madrid .

Chelsea Kukamilisha Usajili Wa Kiungo Wa Monaco ya Ufaransa , Bakayoko  siku ya Kesho huku Ikisemekana Huenda wakapiga   " Double tap in one top of bottom " Kwa kumsainisha Alex Sandro .

Malaga Imenasa Saini ya miaka 3 ya  Adrian Gonzalez akitokea Eibar .

Klabu ya arsenal inaanda ofa Kwaajili ya kunasa Saini ya beki Wa Klabu ya OGC Nice , Jarden Dalbert .

Wesley Sneijder huenda Akatimkia ndani ya Klabu ya sampdoria ya nchini Italia Mara baada ya Kuingia makubaliano na Wakata Ufuta hao Wa Jiji la Italia .

Suso Wa Ac Milan amesema kwamba mpaka sasa amepokea ofa kubwa 3 toka katika Vilabu vinavyoshiriki Ligi ya mabingwa BARANI Ulaya , lakini ameamua Kubaki kuichezea Ac Milan msimu Ujao .

FC Barcelona imefikia makubaliano na Klabu ya Real betis Ili kuwauzia kinda wake , Christian Tello  Huku € 7M zikiwa ada ya Uhamisho wake na atakula kandarasi ya miaka 4 .

Baada ya Juventus Kuthibitisha kwamba Dani alves anaihama Klabu hiyo , Manchester  City imesema ipo tayari kutoa dau lolote ili kunasa Saini ya mkali huyo.

Westbrom inasubiri majibu toka Klabu ya Intermilan mara baada ya kupeleka dau la € 5M ili kunasa Saini ya beki , Andrea Ronacchia .

Baada ya Dani alves Kutimka ndani ya Juventus , Klabu hiyo imeandaa ofa ya € 15M + Bonus ili kunasa Saini ya Danilo Wa Real Madrid kama mziba pengo hilo .

Manchester City wapo katika meza ya mazungumzo na klabu ya Tottenham ili kuangalia Uwezekana Wa kunasa Saini ya beki wake , Kyle Walker .

Klabu za FC Barcelona na Manchester City wote wapo katika mbio za kutaka kunasa Saini ya Ousmane Dembele Wa Borussia Dortmund , Dortmund wamesema thamani ya mchezaji huyo ni € 85M .

Klabu ya Liverpool imesema kwamba bado watahitaji Saini ya Aubameyang ili kujiimalisha zaidi , Kuhusiana na Upande Wa beki Klabu hiyo imesema IPO katila rada za hali ya Juu ili kuangalia Kifaa Kitakacho stahiki  Kujenga Ukuta Wa Klabu hiyo .

Belhanda na Bafetimbi Gomis ni Mali ya Galatasaray kwa  sasa .

Jermain Defoe ni Mali ya Bournemouth .

Fabio Borini ni Mali ya Ac Milan kwa sasa .

Kupata habari zetu Bure kila siku Download Application yetu Bure GUSA HAPA pia usikose kutufatilia kila siku SISI NI SOKA TUNAENDELEA KUKUJUZA.

Comments

Popular posts from this blog

KOSCIELNLY AIBUA HOFU ARSENAL