Ungana nasi kila siku kupata Habari za Michezo,Usajili pamoja na Habari nyingine nyingi
Breaking news
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
#Habari:Watu 12 wamefariki,na wengine 19 kujeruhiwa baada ya basi la New Force lililokuwa likitoka Dar kwenda Songea kupinduka baada ya kugongana na lori uso kwa uso huko kifanya mkoani Njombe usiku wa kuamkia leo.
Mlinzi wa Klabu ya Arsenal Laurent Koscielny anatarajiwa kufanyiwa vipimo ili tatizo lake lijulikane kutokana na kuhisiwa amevunjika taya katika kipigo cha mabao 3-1 ilichopata Arsenal mbele ya Manchester United jana kwa mujibu wa Meneja wake Unai Emery. Koscielny alipigwa kiatu cha uso na mshambuliaji Romelu Lukaku na kushindwa kuendelea na mchezo nafasi yake ikachukuliwa na Matteo Guendouzi katika dimba la Emirates. Emery anaumiza kichwa juu ya walinzi wake kufuatia Sokratis Papastathopoulos kuumia enka kwenye mchezo huo ambapo wanaungana na Hector Bellerin na Rob Holding ambao watakuwa nje ya uwanja kwa msimu mzima. Baada ya kumalizika kwa mechi hiyo Emery alitoa taarifa juu ya Koscielny na Sokratis mbele ya Waandishi wa habari akisema: "Nadhani Sokratis hajaumia sana. "Labda Koscielny itakuwa zaidi inabidi kufanyiwa vipimo nadhani amevunjika kidevu au taya lakini sina uhakika mpaka nipate ripoti ya daktari,". Install /Update Application ya Nijuze Haba...
Comments
Post a Comment