HOJA ZA M600 NA M80 NI HOJA DHAIFU SANA........
-Klabu ya Yanga Sc leo itacheza mchezo wa marudiano wa mtoano wa Caf Confederation Cup na timu ya Welayta Dicha ya Ethiopia mchezo wa mkondo wa kwanza klabu ya Yanga ilishinda kwa magoli 2-0 -Yanga inahitaji kutofungwa zaidi ya goli moja na Dicha ili iweze kufuzu hatua ya makundi ya Caf Confederation Cup iwapo Klabu ya Yanga Itafuzu Makundi ya Kombe hili itapata kitita cha milioni 600 za kitanzania kama zawadi ya kufanikiwa kutinga makundi. -Sasa kumeibuka dhana ya Hoja ya kwamba eti bora milioni 600 kuliko milioni 80 unajua wamaanisha nini bora kufuzu makundi ya kombe la shirikisho wapate milioni 600 kuliko kuchukua ubingwa wa Tanzania Bara (vpl) maana Bingwa wa ligi kuu Tanzania Bara anapata milioni 80. -Ni hoja Dhaifu muno na ni Mbinu za kisungura ambazo kwa watu wa mpira zinatakiwa kuzikataa kata kata huwezi ukasema bora milioni 600 kuliko milioni 80 wakati ushindi wa milioni 80 ndio uliofanya timu izifikie hizo milioni 600 huwezi kucheza makombe ya Afrika bila kushin...